ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 17, 2023

"VIJANA MKIPATA MIKOPO YA SERIKALI KWA VIKUNDI HUU HAPA UWEKEZAJI WENYE UHAKIKA"

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

WATANZANIA wametakiwa kuanza kilimo cha Vannila kwani zao hilo lina soko na bei kubwa katika mataifa yenye uchumi mkubwa duniani hivyo lina uwezo wa kumwinua mkulima haraka na husistawi kwa muda mfupi.

Wito huo umetolewa Jijini Mwanza na Mkurugenzi Mtendaji wa Vanilla International Ltd Simon Mnkondya katika semina za kufungua fursa zitokanazo na kilimo hicho katika Kanda ya ziwa.

Amesema licha ya zao hilo kuwa na maslahi makubwa ya kumwezesha mkulima kujikomboa kimaisha vilevile ni rafiki wa mazingira hata hivyo mpaka sasa Kanda ya ziwa ni wakaazi asilimia 0.02 ndo wanalima zao hilo.

Mnkondya ameongeza kuwa zao hilo huchukua mwaka mmoja tangia kupandwa hadi kuvunwa huku kilo moja inauzwa sh 1,000,000/= na inatumika katika kutengenezea pafumu nzuri, vipodozi,hutumika kutengenezea juisi, pipi, soda na kutibu magonjwa kama kansa.

Mpaka sasa bado watanzania wengi hawajazichangamkia fursa za uwekezaji wenye tija kwa kulima zao la vanilla hali inayopekelea kuwa na maeneo machache yaliyolimwa zao hilo, mikoa na maeneo kama 
Zanzibar, Kwimba, Arusha, Kilimanjaro,Singida, Daressalaam,Bagamoyo, Kibaha na Ubungo.


Mkaazi wa Jiji la Mwanza Dolla Ng’wandu ameiomba serikali kuangalia fedha zinazotolewa kwa makundi ya vijana toka kwenye halmashauri zao watumie kwa kilimo cha vanilla kutokana na kuwa na bei kubwa kwenye soko ili waweze kupata manufaa.

Amesema mikopo hiyo kwa vijana ambayo imekuwa ikitolewa na halmashauri zao mara kwa mara haina tija ya kuwainua kiuchumi ambapo pia hupotea kutokana na mzunguko kuwa mgumu hivyo ameshauri kutokana na ujio wa fursa kwa zao la vanilla hakuna budi kusaidiwa vijana waendeshe kilimo hicho kwa sasa.

Mkulima kutoka Mkoani Simiyu, Bayege Mbugani ambaye alikuwa ni mfugaji wa ng’ombe na kwa muda amekuwa akihamahama kutafuta marisho hadi kufika mikoa ya Kusini lakini baada ya kupata kufahamu fursa ya zao la vanilla ameachana na ufugaji wa namna hiyo.

“Naomba serikali isaidie wakulima kupata urahisi wa kupata utaalam wa kilimo hicho ili walime kwa mafanikio makubwa tofauti na ilivyo kwa sasa” alisema Mbugani.

Amesema kuwa mpaka sasa anamiezi saba tangu awekeze kwenye zao hilo na faida ambayo ameipata ikiwemo kuuza matawi ya vanilla futi 2 kwa kiasi cha shilingi 20,000, kwa muda

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.