ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 25, 2023

KUNGUNI WADHIBITIWA MV VICTORIA 'SASA KUNA KITENGO MAALUM CHENYE WATAALAM WA AFYA'

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Afisa uhusiano wa kampuni ya huduma za meli nchini (MSCL), Edmond Rutajama amekutana na kufanya kikao kazi na waandishi wa habari wa mkoa wa Mwanza kutoa taarifa za miradi inayoendelea kutekelezwa na kampuni hiyo ikiwemo ujenzi wa meli ya Mv. Mwanza Hapa Kazi Tu.


Pamoja na hayo afisa huyo ametumia muda huo kujibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari likiwemo lile la muda mrefu ambalo kwa kipindi fulani lilizua gumzo mitandaoni na kuleta sintofahamu iliyokosa majibu, kwamba moja ya meli zake Mv Victoria imekuwa mazalio ya kunguni mende na viroboto nao abiria wakijiuliza , uchafu huo unasababishwa na nini?  Jeh wahusika, hawalioni hilo? Na jeh hatua zipi zimechukuliwa mpaka hivi sasa kudhibiti hali hiyo?


Rutajama amesema, Mwaka wa fedha 2022/2023 serikali imetenga shilingi bilioni 113,706,822,200 kwa ajili ya kutekeleza miradi  12 ya meli, miradi 4 ikiwa mipya, 5 ikikarabatiwa  na  miradi 3 ikitekelezwa.


Ziwa Tanganyika zitatumika bilioni 53 kutekeleza miradi 7, na bilioni  57 zitatumika kutekeleza mirdi 5 ndani ya ziwa Victoria huku bilioni 2 zitatumika kuendesha meli 3 zilizopokelewa kutoka Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA). Edmond Rutajama  Afisa Uhusiano (MSCL )

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.