ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 10, 2022

WAZIRI DR CHANA AFUNGUA MAONYESHO YA UTALII KARIBU KUSINI MKOANI IRINGA.

 

 

Waziri wa maliasiali na utalii Balozi Dkt Pindi Chana amefungua maonyesho ya pili ya kimataifa ya karibu kusini kata viwanja vya kituo cha kikuu cha utalii kusini Kihesa Kilolo mkoani Iringa ikiwa na lengo la kutangaza vivutio vya kitalii vilivyo kusini.

Waziri wa maliasiali na utalii Balozi Dkt Pindi Chana akiteta jambo na mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya pili ya kimataifa ya karibu kusini kata viwanja vya kituo cha kikuu cha utalii kusini Kihesa Kilolo mkoani Iringa ikiwa na lengo la kutangaza vivutio vya kitalii vilivyo kusini.



Na Fredy Mgunda,Iringa.

WAZIRI wa maliasiali na utalii Balozi Dkt Pindi Chana amefungua maonyesho ya pili ya kimataifa ya karibu kusini kata viwanja vya kituo cha kikuu cha utalii kusini Kihesa Kilolo mkoani Iringa ikiwa na lengo la kutangaza vivutio vya kitalii vilivyo kusini.

akihutubia wananchi waliojitokeza wakati wa kufungua maeonyesho hayo, waziri wa  Balozi Dkt Pindi Chana alisema kuwa imefika zamu ya kuvitanga vivutio vya kitalii vilivyo kusini ili kuongeza watalii kutembelea na kuongeza pato la taifa.

Balozi Dkt Chana alisema kuwa serikali itatumia maonyesho ya kimataifa ya karibu kusini kama sehemu ya mkakati kutekeleza ilani ya CCM ya kufikisha watalii milioni tano ifikapo mwaka 2025 na wizara ya maliasili imejipanga kimkakati ili kufikia malengo hayo na ikiwezekana kuvuka idadi hiyo ya watalii.

alisema kuwa maonyesho hayo yamefunguliwa rasmi yakihusisha mikoa kumi ya kusini mwa Tanzania ikiwa ni sehemu muafaka yakutangaza utalii wa kusini.

Balozi Dkt Chana alisema kuwa mikoa inayoshiriki maonyesho hayo ni mkoa wa Iringa,Morogoro,Njombe,Mbeya,Songwe,Rukwa,Katavi,Ruvu Lindi na Mtwara ,mikoa hiyo kwa kutumia maonyesho hayo itasaidia katika kutangaza vivutio vya utalii kusini mwa Tanzania.

alisema kuwa maonyesho hayo ya karibu kusini yenye kaulimbiu inayosema “uwekezaji,kusinifahari yetu”ni jukwaa ambalo linawakutanisha wadau mbalimbali katika sekta ya utalii kwa lengo la kuuza bidhaa,kutafuta masoko pamoja na kujenga mahusiano ya kibiashara kwenye sekta mbalimbali za kitalii..

Balozi Dkt Chana alisema kuwa kutokana na kampeni ya filamu ya Tanzania The Royal Tour ilifanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kumesaidia kuongeza idadi ya watalii wa kimaoka watalii 922,692 mwaka 2019 hadi kufukia watalii 1,034,180.

alisema kuwa mikoa ya nyanda za juu kusini imebarikiwa kuwa na vivutio vingi vya kitalii hivy kupitia mradi wa REGROW utasaidia kuvitangaza vivuti hivyo na kujenga kituo cha utaliiwa kusini mwa Tanzania katika eneo la kihesa Kilolo ambacho kitatumia zaidi ya bilioni 12.

Balozi Dkt Chana alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imeendelea kujenga viwanja vya ndege kwa lengo la kukuza na kuitanga sekta ya utalii ili kuongeza idadi ya watalii wa ndani na nje ya Tanzania.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.