ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, August 2, 2022

NANE NANE MWANZA 2022 FASTA PAMEANZA KUNOGA

 Maadhimisho ya Sikukuu ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi (Nane Nane) yalianza rasmi Mwezi Agosti mwaka 1994 na yamekuwa yakiadhimishwa Kitaifa kwenye Kanda Nane (8) kama ifuatavyo: –

Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, uwanja vya John Mwakangale, Uyole, Jjijini Mbeya; Kanda ya Kaskazini, uwanja wa Themi, Jijini Arusha; Kanda ya Mashariki, uwanja wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Manispaa ya Morogoro; Kanda ya Ziwa, uwanja wa Nyamhongolo, Jijini Mwanza; Kanda ya Kati, Uwanja wa Nzuguni katika Jiji la Dodoma; Kanda ya Magharibi, Mkoani Tabora katika uwanja wa Ipuli; Kanda ya Ziwa Mashariki, Mkoa wa Simiyu katika uwanja wa Nyakabindi na mwisho ni Kanda ya Kusini, Mkoani Lindi katika uwanja vya Ngongo.

Ikiwa leo ni siku ya pili tu lakini tayari wajasiliamali, mashirika na taasisi mbalimbali binafsi na zile za Serikali tayari wamekwisha simika mabanda yao kwenye viwanja hivi kwaajili ya kushiriki maonesho haya. Moja kati ya vivutio vikubwa hambavyo huwavuta watu hata wakahudhuria kwa wingi ni masuala ya misosi na zile chomachoma, askwambie mtu zipo za kutosha nazo zikipatikana kwa bei rahisi kuliko hata zile bei zetu za kitaa. Hatua chache Napata nafasi ya kuzungumza na wadau wa banda la masuala nyeti ya fedha … Nazungumzia Benki Kuu ya Tanzania tawi la Mwanza….

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.