ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 17, 2022

KANUNI ZA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI MTANDAONI ZAPITIWA NA KUTHIBITISHWA.

  Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari nchini Tanzania (UTPC) umekutana na Waandishi wa Habari Mtandaoni (Bloggers/Youtubers) kwa ajili ya kupitia na kuthibitisha Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni na Vyombo vya Habari vya kawaida.

Mkutano huo umefanyika leo Ijumaa Juni 17,2022 katika ukumbi wa Adden Palace Jijini Mwanza na kuhudhuriwa na waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii kutoka mikoa mbalimbali. Akifungua Mkutano huo, Mkurugenzi wa UTPC, Abubakar Karsan amesema Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni zitasaidia kupunguza wimbi la habari za uongo mtandaoni hivyo kupunguza malalamiko mbalimbali.

Mshauri Mwelekezi wa Kutengeneza Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni, Pili Mtambalike akizungumza kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni.
Mshauri Mwelekezi wa Kutengeneza Kanuni za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni, Pili Mtambalike akizungumza kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakiwa kwenye Mkutano wa Kupitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakipitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakipitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 
Waandishi wa habari wa mitandao ya Kijamii wakipitia na Kuthibitisha Kanuni  za Maadili ya Uandishi wa Habari Mtandaoni 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.