ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 2, 2022

WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI WAONYWA WEREDI WIZI WA MITIHANI.

 


Afisa elimu mkoani Mara, Benjamini Oganga amewataka wakuu wa shule za sekondari kufanya kazi kwa nguvu zote weledi,bidii,ujuzi zaidi ili watoto wetu na ndugu zetu wapete kupata elimu bora na kuinua ufaulu bila kuiba mitihani.


Afisa huyo aliongeza kusema kuinua ufaulu kuanzia shuleni hadi ngazi ya mitihani ya Taifa lengo lake ni pale ambao wataende kufuta matokeo ya alama ya ufaulu ya Division (0) na (4).


Katika hatua nyingine Afisa huyo alisema kuwa walimu wakuu wanapaswa kuwa na mbinu za kuhakikisha wanafunzi wanakaa kwenye mfumo wa elimu na kuwa wanaanza kupima wakuu wa shule kwa usimamizi wa wanafunzi na walimu ambapo amesisitiza lugha ya Kingereza katika shule za sekondari Mkoani hapa.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa wakuu wa Shule TAHOSSA Mkoani hapa,Magudira Mugeta amezitaja sababu baadi zinazowakabili wakuu wa shule kadhaa na pia kuchangia kwa ufaulu wa watahiniwa kushuka madaraja kwa shule za sekondari mkoani hapa.


“Mheshimiwa mgeni rasimi pamoja na kufanya kazi kwa bidii yapo mambo machache yanayoleta changamoto na kurudisha nyuma juhudi za kuinua kiwango cha cha elimu mkoani hapa kama vile wakuu wa shule kutochangia ada za TAHOSSA kwa wakati kwa ngazi zote,baadhi ya wakuu wa shule kutohudhuria vikao hivi ambavyo ni vya mhimu katika usimamizi wa shule maana maelezo na maelekezo mbalimbali ya serikali hutolewa katika vikao hivi na kukosekana kwa semina(Orientation/workshop)kwa wakuu wa shule ambao niwateule wa hivi karibuni”alisema Mageta.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Professor Mwera Faundation,Hezeboni Mwera ambao pia ni wadau wa elimu alisema wameanzisha mpango wa kutoa tuzo kwa shule ndani ya mikoa kumi hapa Tanzania.


Mwera aliongeza katika kikao hicho kuwa  wamefadhili chakula cha wageni ikiwemo kutoa ukumbi wa mkutano bure na kuongezakuwa wakuu wahao shule za sekondari wajihadhari na matapeli wanaofika mashuleni wakitaka wanafunzi kujiunga na vyo mbalimbali vya veta ambavyo havikusajiliwa kisheria.


Nasisitiza kuweni makini na watu wanakuja kweny shule kwani baadhi ya vyuo havijasajiriwa na sasa tunashukuru serikali imeunganisha vyuo vyote kuingia katika mfumo wa NACTE alisema Mwera.


Katika kikao hicho cha TAHOSSA kilichokalia ukumbi wa Taasisi ya Professor Mwera Faundation ilitajwa kuwa asilimia 69 ya wanafunzi wakike mkoani hapawanashindwa kumaliza masomo.


Afisa Elimu Taaluma Mkoa wa Mara,Ayubu Mbilinyi alisema kuwa Idadi kubwa ya wanafunzi katika Mkoa wa Mara wanatajwa kutomaliza masomo yao ya sekondari tangu pale wanapoandikishwa hususani wasichana.


ambapo wanafunzi zaidi ya elfu tisa wanatajwa kupotea ambapo asilimia 69 ni wasichana.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.