ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 2, 2022

MOTO WATEKETEZA MADUKA 520 SOMALILAND

 


Mamlaka ya jimbo lenye kutaka kujitenga la Somalia, Somaliland imesema moto uliozuka ghafla jana jioni umeteketeza maduka 520, maghala na ofisi za masoko ya jumla. 

Moto huo ulioliteketeza soko kubwa la Waheen, mjini Hergeisa, ulisambaa umbali wa kilometa 5.Ulishindikana kuzimwa hadi mapema leo. 




Akielezea mkasa huo, Meya wa mji wa Hargeisa, Abdikarim Ahmed Mooge alisema hilo ni tukio baya zaidi la moto kuikumba Somaliland.

Somalind ilijitangazia uhuru wake kutoka kwa Somalia 1991 lakini halijatambuliwa kuwa taifa na jumuiya ya kimataifa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.