ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 25, 2022

RAIS SAMIA; WAFUNGWA WANAWEZA KUITWA WANAFUNZI.

 


Rais Samia Suluhu Hassan amesema, wanaohukumiwa kufungwa jela wanaweza kupewa jina la wanafunzi kwa sababu shughuli kubwa ya Magereza ni pamoja na kujifunza na kurekebisha watu.


Amesema hayo leo Ijumaa Machi 25, 2022 katika uzinduzi na uwekaji wa mawe ya msingi kwenye miradi ya makao makuu ya Magereza jijini Dodoma.


“Ni kweli kabisa ndugu zetu wanaohukumiwa kufungwa ni wafungwa, lakini tunaweza kuwapa jina la wanafunzi kwa sababu shughuli kubwa ya Magereza pamoja na adhabu ni kujifunza na kurekebisha watu kwa shughuli wanazojipanga nazo,”amesema Rais Samia Suluhu Hassan


“Wakishirikishwa ipasavyo inakwenda kuwapa uzoefu na kwenda kuwapa taaluma, wakitoka waende kujitegemea haitaeleweka kama mfungwa anatoka hana la kufanya kama wale tulizoea kuwaona wakati wa msamaha,”amesema.


“Mfungwa anasamehewa leo nje hana la kufanya hana pa kukaa familia inamkana. Anaamua kwenda tena kuiba kwa makusudi ama kwenda kufanya jambo ambalo ataonekana kufanya akamatwe arudishwe tena. Huo sio mwendo mzuri mwendo mzuri ni wanafunzi hawa wanapotoka kwenda kuweza kujitegemea kutokana na taaluma na ujuzi watakaokuwa wanapata wakiwa ndani,”amesema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.