ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 24, 2022

RAIS SAMIA ATAKA KUONDOLEWA KWA ALAMA YA MWENGE KATIKA DARAJA LA TANZANITE.

 

Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amemwagiza Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa kubadilisha alama ya mwenge iliyowekwa kwenye daraja mpya la Tanzanite na kuweka alama ya madini hayo itakayoendana na jina la daraja hilo.

Hayo ameyasema leo Machi 24, 2022 Dar es Salaam kwenye hafla ya uzinduzi wa daraja hilo lilogharimu Sh 243 bilioni.

Rais Samia amesema ushauri huo aliupata kutoka kwa wananchi kwamba wangependa daraja hilo walipoweka alama ya mwenge, basi kuwekwe alama ya Tanzanite ili kuendana na uhalisia wa jina la mradi huo.

“Niseme kidogo Waziri ushauri nilioupata kutoka kwa wananchi daraja hili tunaliita la Tanzanite lakini alama tuliyoiweka ni alama ya mwenge. Pamoja na kutambua mwenge ni tunu yetu adhimu wananchi wangependa sana kuona alama ya tanzanite pale ilipo alama ya mwenge ili liendane na jina la daraja hili,” amesema Rais Samia.  
Hata hivyo, Rais ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi kushiriki kikamilifu katika sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika mwaka huu.

“Nitoe wito kama ilivyo kawaida yangu kujitokeza kwa wingi wakati wa kuhesabiwa Agosti mwaka huu, twendeni tukahesabiwe,” amesema.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.