ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 19, 2022

BIDEN AMTAKA RAIS XI WA CHINA KUITOISAIDIA URUSI.

 


Rais wa Marekani Joe Biden amemuonya mwenzake wa China Xi Jinping juu ya athari zitakazoikabili Beijing, endapo itatoa msaada wa vifaa kwa Urusi katika uvamizi wake nchini Ukraine. 

Biden ametoa onyo hilo wakati wa mazungumzo kwa njia ya video na rais Xi juu ya mzozo wa Ukraine. 

Msemaji wa Ikulu ya Marekani White House Jen Psaki, amesema rais Biden ameelezea jitihada za Marekani na washirika wake katika kushughulikia uvamizi wa Urusi, ikiwemo kuiwekea vikwazo vikali Moscow. 

Wizara ya mambo ya nje ya China imeandika kwamba rais Xi amemueleza Biden, juu ya kukomeshwa vita ya Ukraine haraka iwezekanavyo na kutoa wito kwa jumuiya ya kujihami NATO kufanya mazungumzo na Moscow, ili kushughulikia kiini cha mzozo wa Ukraine na kupunguza wasiwasi wa usalama wa mataifa hayo jirani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.