ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, March 20, 2022

ANUSURIKA AJALI ILIYOUA 23 AKIENDA TANGA KUJIFUNGUA.

 


ZAHARA  Shaaban (31), ambaye ni mjamzito, ameshukuru  namna alivyookolewa na msamaria mwema kutoka kwenye basi lililopata ajali kwa kupitishwa dirishani .


Mama huyo ni miongoni mwa majeruhi 26, waliolazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro, baada ya kutokea kwa  ajali ya basi  la Ahmeed Coach, lilokuwa likitokea  mkoani Mbeya  kwenda  jijini Tanga na kusababisha vifo 23.


Zahara amezungumza na kusema yeye ni mzaliwa wa Tanga, lakini  ameolewa mkoani  Iringa  na alikuwa anasafiri na basi hilo kwenda nyumbani kwao,  eneo la Mwanzange au kwa jina lingine  Mwakazalu, Tanga  kusubiri muda wa  kujifungua.


“ Kutokana na hali yangu hii  ya kuelekea kujifungua, nilionelea bora niende kwetu nyumbani Tanga, kujisubiria kujifungua, “ amesema  Zahara.


Anasema  alipata siti ya kukaa kwenye basi hilo, lakini alisema kuna mua alikuwa amechoka, hivyo kuamua kulala chini kwenye ‘korido’ ya basi hilo.


“ Wakati  hii ajali  inatokea sikuweza kujua au kuona  kilichotendeka  zaidi ya kushituka baada ya kutokea kishindo, kikubwa na kuangukiwa  na mizigo  iliyowekwa pembezoni ndani ya basi hili,” amesema.


Mizigo  hiyo ilimwangukia kwenye mguu wa kulia na kifuani pamoja na abiria aliyekua kwenye siti ya karibu yake alipokuwa amelala chini, ambaye alimlalia juu.


 “ Mtu mmoja  amenisaidia kwanza kumtoa aliyenilalia, kunichomoa na kunitoa kupitia kwenye dirisha  na nikapokelewa nje ya dirisha na mfugaji wa Kimasai, wakanilaza chini kwenye majani nipate hewa na nikaingizwa kwenye gari hadi hospitalini  


“  Nawashukuru madaktari na waauguzi,  nimevunjika mguu wa kulia  kwenye kifundo …nilipata  maumivu ya kifuani na michubuko midogo mguu wa kushoto,” amesema  Zahara.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Fortunatus Musilim ameeleza  ajali hiyo  ilitokea  jana Machi 18,  saa 10 alasiri na  chanzo ni dereva wa Lori lenya namba za IT 2816 likitokea  Dar es Salaam kwenda  nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), lililokuwa linamkwepa mwendesha pikipiki, hivyo kugongana uso kwa uso na basi ya Ahmeed  lenye namba T 732 ATH .

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.