ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 18, 2021

USALAMA WAIMARISHWA KAMPALA BAADA YA MASHAMBULIZI YALIYOUA WATU 6

 


Usalama umeimarishwa katika mji mkuu wa Uganda Kampala, siku moja baada ya mashambulizi mawili ya mabomu kuutikisa mji huo na kusababisha vifo vya watu sita.

Maafisa wa polisi na wanajeshi waliojihami wameonekana wakishika doria katika maeneo mbalimbali ya mji huo/

Wito umetolewa pia kwa raia nchini humo kuwa katika hali ya tahadhari kufuatia mashambulizi ya jana, ikiwa ndiyo ya hivi karibuni zaidi katika mfululizo wa mashambulizi ambayo yameshuhudiwa siku za hivi karibuni.

Kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS limedai kuhusika na shambulizi hilo la kujitoa muhanga lililolenga kituo cha polisi na majengo ya bunge.Zaidi ya watu 33 walijeruhiwa kwenye mashambulizi hayo ya jana.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.