ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 18, 2021

UPUNGUFU WA UMEME, TANESCO KUGEUKIA GESI ASILIA.

 


Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), limesema linachukua hatua za haraka kwa kuongeza uzalishaji kwa kutumia gesi asilia.

Hatua hizo ni kutokana na mabadiliko ya hali hewa, kupungua kwa kiwango cha maji katika mito na mabwawa nchini.

Taarifa ya Tanesco iliyotolewa leo Alhamisi Novemba 18, 2021 imesema hali ya upungufu huo imeathiri uzalishaji katika vituo vya kuzalishia umeme vinavyotumia maji.

“Athari kubwa imetokea katika vituo vyetu vya Kihansi, Kidatu na Pangani. Jumla ya upungufu wa uzalishaji ni nakribani megawati 345 ambayo ni asilimia 21 ya uzalishaji wote” imesema.

Hata hivyo shirika hilo limesema linachukua hatua za haraka kuongeza uzalishaji kwa kutumia gesi asilia kwa kuharakisha matengenezo ya baadhi ya mitambo yake ya Ubungo I inayozalisha megawati 25.

Vituo vingine ni Kinyerezi I megawati 185, Ubungo III megawati 112, pamojqa na kuwasha kituo cha Nyakato kinachozalisha megawati 36 hali itakayofanya kuwa na jumla ya megawati 358.

 “Kwakuwa kutakuwa na upungufu kwa baadhi ya mikoa taarifa zitatolewa kwa wakati ili wateja waweze kupanga kazi zao”. Imeeleza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.