ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, February 27, 2020

WANAFUNZI WALIOLAZIMIKA KUPANGA NYUMBA ZA WAGENI ILI KUPATA ELIMU SASA BASI.


Ni katika ziara ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Mwanza Dkt. Anthony Diallo kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali kama sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM mwaka 2015 - 2020. Dkt. Diallo akiwa wilayani hapa kwenye ziara ya Chama hicho akiiongozana na kamati ya siasa ya CCM mkoa wa Mwanza anashiriki ujenzi wa shule ya sekondari Sukuma inayojengwa wilayani Sengerema kwa fedha za Wananchi wakishirikiana na Serikali ambapo licha ya kuwapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu katika kuisaka elimu pia hatua hiyo imewanusuru kukatisha masomo kutokana na kushindwa kumudu gharama sanjari na mimba. Shule ya sekondari Sukuma inatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi Mwezi April mwaka 2020.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.