ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 9, 2020

KITUO CHA PILI NCHINI CHA KUPIMA NA KUHAKIKI MATENKI YA MALORI YA MAFUTA CHAANZA KUFANYA KAZI MWANZA



WAMILIKI wa Malori ya kubeba mafuta kwa mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Kagera, Simiyu, Geita na mikoa jirani na Kanda ya Ziwa sasa hawato ingia gharama ya kuchoma mafuta kusafirisha maroli yao hadi jijini dar es salaam kwaajili ya kupata huduma ya upimaji na uhakiki matenki yao kila mwaka mara baada ya Serikali kusimika kituo cha kisasa cha upimaji katika eneo .la Nyamhongolo wilayani Nyamagana jijini Mwanza. Hiki ni kituo cha pili cha upimaji matenki ya magari ya kubebea mafuta nchini kikitanguliwa na kile cha jijini Dar es salaam. Meneja wa wakala wa vipimo mkoani Mwanza Arobogast Kajungu anasema malengo ya Serikali katika kuwahudumia wafanyabiashara wa mafuta Kanda ya Ziwa yametimia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.