ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 28, 2020

KITUO CHA KUKUZA BIASHARA ZA WAJASILIAMALI CHAZINDULIWA JIJINI MWANZA.


Tanzania kuelekea nchi ya uchumi wa kati ifikapo 2025 ni suala ambalo mgombea urais kupitia tiketi ya CCM katika uchaguzi mkuu uliofanyika 2015, Dk John Magufuli alikuwa akilihubiri kila alipokuwa akisimama katika mikutano ya hadhara.

Alieleza kwamba serikali atakayoiunda akipewa ridhaa hiyo amekusudia iwe ambayo itabadili maisha ya watanzania hususani wale wenye kipato cha chini, katika mwendelezo wa juhudi za kufanikisha adhma hiyo Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella amezindua kituo cha kuendeleza ukuaji wa biashara za wajasiriamali kupitia shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) chini ya mradi wa SIDO TLED HUB, 

Mongella amefanya uzinduzi huo Januari 24, 2020 katika viunga vya ofisi za SIDO Nyakato jijini Mwanza na kubainisha kwamba serikali mkoani Mwanza iko tayari kutoa ardhi kwa ajili ya shughuli za viwanda vidogo.


 Mkurugenzi Mkuu SIDO, alisema Profesa Sylvester Mpanduji akizungumza kwenye uzinduzi huo.
 Meneja SIDO Mkoa Mwanza, Bakari Songwe akitoa salamu zake kwenye uzinduzi huo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC), Mariam Munanka akitoa salamu zake kwenye uzinduzi huo.
 Rais wa chama cha wafanyabiashara, viwanda na kilimo TCCIA, Paul Koyi akizungumza kwenye ufunguzi huo.
Mkurugenzi Mkazi Shirika la VSO, Dawn Hoyle akitoa salamu zake kwenye mkutano huo.
Mwakilishi Ubalozi wa Canada nchini Tanzania, Christopher Duguid akitoa salamu zake kwenye uzinduzi huo.
Mwakilishi shirika la Africa CUSO International, David Forest akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Mwakilishi Mkazi Shirika la Africa CUSO International, Romanus Mtunge akitoa salamu zake kwenye uzinduzi huo.
 Wadau mbalimbali wakifuatilia uzinduzi huo.
 Wadau mbalimbali wakiwemo kutoka Kituo cha Biashara, Viwanda na Kilimo nchini (TCCIA) walikuwa sehemu ya waliojumuika kwenye hafla hiyo.
 Wadau kwa umakini na tafakari wakifuatilia hafla hiyo.

 Wadau kwa umakini na tafakari wakifuatilia hafla hiyo.
 Mkurugenzi wa kampuni ya Mwanza Quality Wines inayotengeneza mvinyo wa matunda (Power Banana), Leopord Lema (kulia) akitoa ufafanuzi kuhusiana na bidhaa hiyo baada ya Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kushoto) kutembelea mabanda ya wajasiriamali mbalimbali waliohudhuria halfa hiyo.
 Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kushoto) akifurahia jambo baada ya kutembelea banda la kampuni inayotengeneza mvinyo kwa kutumia ndizi jijini hapa ijulikanayo kama  Mwanza Quality Wines.

Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (kushoto) akiwa banda la wajasiliamali akinamama.

"Wote ni mashahidi kwamba kuna baadhi ya wajasiliamali kupitia mikopo wameuziwa nyumba zao, viwanja vyao hata mali zao walizokuwa nazo, wamesaidiwa kuanzisha mpango wa biashara unaouzika benki na kukopesheka lakini hawakusaidiwa mpango unaolingana na wazo la mwenye biahsra na muelekeo wa mfanyabiashara. Kituo hiki kitahakikisha wajasiliamali wanapata mikopo inayofanana na wao, kuwaelekeza maeneo yanayotakiwa sanjari na masoko yanavyohitaji"  alisema Mwakilishi Mkazi Shirika la Africa CUSO International, Romanus Mtunge akitoa salamu zake kwenye uzinduzi huo.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.