ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, January 13, 2020

BODABODA WAFURAHIA SERIKALI KUWAKUMBUKA KUINGIZWA MFUKO WA BIMA YA AFYA (NHIF)


Jumuiya za Wajasiriamali wadogowadogo na Waendesha Bodaboda nchini wamepongeza hatua ya kuanzishwa kwa vifurushi vya bima ya afya ambavyo vimewawezesha katika kupata matibabu ya uhakika pindi wanapoumwa. Wakiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya Bima ya Afya viongozi wa jumuiya hizo wamesema ilikuwa ni hitaji lao la muda mrefu la kuhakikisha wanachama wao wanakuwa na uhakika wa matibabu kwa kuwa na bima za afya. Aidha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Mhe. Anne Makinda akiongea wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiunga na vifurushi vya bima ya afya Mkoani Mwanza, ambapo alisema mpango wa vifurushi umekuja kwa ajili ya kuwajumuisha watanzania wote.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.