ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 4, 2019

STEVE NYERERE ASIMULIA MAAJABU YA BURIGI NA KISIWA CHA SAANANE ALIPOITWA NA MAMBA.



Mwishoni mwa wiki Mabalozi wa Uzalendo Kwanza Tanzania walitembelea hifadhi mbalimbali Kanda ya Ziwa ikiwemo Burigi Chato, Rubondo, Ibanda na kumalizia utalii wao kisiwa cha Saa Nane. Wakiwa wameambatana na waziri mwenye dhamana ya sekta husika, Waziri wa Mali Asili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla na wasanii hao akiwemo maarufu wa wa maigizo na komedi Steve Nyerere amesimulia maajabu aliyokutana nayo.
Kisiwa cha Saanane (Saanane Island National Park) ni hifadhi ya taifa la Tanzania na ni hifadhi ndogo yenye eneo la kilomita za mraba 2.18, na iko umbali wa kilometa 2 kusini magharibi kutoka katikati ya jiji la Mwanza, katika Ghuba ya Ziwa Victoria nchini Tanzania. Hifadhi hii ilianzishwa kama bustani ya kwanza ya wanyama nchini Tanzania mwaka 1964 ikawa hifadhi kamili mwaka 2013. Lengo la kuanzishwa kwake ilikuwa kuhamasisha uhifadhi wa wanyama na kuelimisha jamii, pamoja na kutoa nafasi kwa wakazi wa Mwanza kupumzika.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.