ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, December 3, 2019

MICHEPUKO KIKWAZO KWA WANAUME WENGI KUGWAYA KUPIMA UKIMWI


WAKATI vita dhidi ya mapambano ya ugonjwa wa Ukimwi ikipamba moto nchini, imebainika kuwa baadhi ya wanaume kuwa na uhusiano wa mapenzi na wanawake wengi ni moja ya sababu inayowafanya waogope kupima virusi vya Ukimwi.

Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (Nacopha), Leticia Kapela, alisema hayo jana, wakati wa maadhimisho ya kilele cha Siku ya ukimwi Duniani mkoani Mwanza.

Amesema kutokana na hali hiyo, wengi wao hujikuta wakisubiri wenzi wao wapime afya zao pindi wanapokuwa wajawazito, ambapo wakiona wako salama na wao huamini kuwa hawana maambuzi ya VVU.

Aidha Bi. Leticia ameongeza kuwa wanaume hao badala ya kupima afya zao, husubiri wake zao kupima afya wanapokuwa wajawazito.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.