ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, December 11, 2019

MWANZO MWISHO WALIVYOACHIWA WAFUNGWA GEREZA LA BUTIMBA MWANZA KWA MSAMAHA WA RAIS MAGUFULI



 Siku moja baada ya Rais wa Tanzania, John Magufuli kuwasamehe wafungwa 5,533 katika maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika, wafungwa 79 kati ya hao waliokuwa wamefungwa katika gereza la Butimba Mkoa wa Mwanza wameachiwa Jumanne Desemba 10, 2019.

Rais Magufuli alitangaza msamaha huo katika maadhimisho hayo, akibainisha kuwa idadi hiyo ni kubwa kuwahi kutokea kuliko wakati mwingine wowote na kutaka walengwa ndio waachiwe.

Katika mkoa wa Mwanza wafungwa watakaopata msamaha huo ni 190.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amefika katika gereza la Butimba kwa ajili ya kushuhudia utekelezaji wa agizo la Magufuli huku mkuu wa gereza hilo, Hamza Hamza akitaja idadi ya watakaoachiwa.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.