ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, December 24, 2019

MAGUFULI AIBUA SHANGWE KRISMASI WAFANYAKAZI WAMTAKA WAZIRI MPINA KUFUNGA NATI UVUVI HARAMU


WAFANYAKAZI wa kiwanda cha kuchakata mabondo cha HONGLIN INTERNATIONAL TRADE DEVELOPMENT cha jijini Mwanza wamepaza sauti zao na kuishukuru Serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli kwa namna ilivyopambana na Uvuvi Haramu na kuwezesha kupatikana malighafi za kutosha zilizowezesha kupatikana kwa ajira ya uhakika viwandani.

Wameitaka Serikali kuendelea kufunga nati ili kuwabana wavuvi haramu ili rasilimali za uvuvi ziongezeke mara dufu na kuwezesha viwanda zaidi kwani sasa ajira zimeongezeka kutokana na ongezeko la samaki.

Waziri wa mifugu na uvuvi, Luhaga Mpina amewahakikishia kuwa Serikali iko imara na itaendelea kulinda rasilimali hizo ili ziweze kutumika kwa manufaa ya Watanzania wote.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.