ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 21, 2019

NMB YAUNGA MKONO SAFARI KUELEKEA WIKI YA MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI KITAIFA MWANZA


"Kama unavyojua NMB ni mdau mkubwa wa shughuli za kijamii, tumekuwa tukisapoti majukumu mbalimbali kama vile vitanda mahospitalini, madawati mashuleni, ujenzi wa madarasa lakini pia harakati mbalimbali za mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi na kusaidia wasiojiweza"    Alisema Amos David Mwabusi ambaye ni mwakilishi wa Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa katika makabidhiano ya T Shirt 400 zitakazotumika kama sare kupamba maadhimisho hayo ambayo kitaifa kwa mwaka huu 2019 yanafanyika mkoani Mwanza.

Siku ya Ukimwi Duniani inaadhimishwa kila tarehe 1 Desemba kama siku maalumu ya kupanua ufahamu kuhusu maafa yanayoletwa na ugonjwa wa Ukimwi.

Desemba mosi ilichaguliwa kuwa siku ya Ukimwi kutokana na tarehe hiyo kuwa ndiyo siku ambayo virusi cha Ukimwi kilitambulika rasmi mwaka 1981. Toka mwaka 1981 hadi 2007 watu zaidi ya milioni 25 wameshafariki kutokana na Ukimwi. Mwaka 2007 peke yake walifariki milioni 2, kati yao watoto 270,000.

Siku hiyo ilichaguliwa rasmi mwaka 1988 wakati wa Mkutano wa Dunia wa Mawaziri wa Afya Kuhusu Mpango wa Kuzuia Ukimwi. Kuanzia hapo siku hiyo imekuwa ikikumbukwa rasmi na serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, na wanaharakati.

Toka mwaka 1988 hadi 2004, Siku ya Ukimwi Duniani ilikuwa ikiratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Ukimwi (UNAIDS). Mwaka 2005 UNAIDS ililipa shirika lisilo la kiserikali la Kampeni ya Ukimwi Duniani (the World AIDS Campaign) wajibu wa kuratibu siku hiyo.

Kila mwaka siku hiyo hufanyika kwa ujumbe maalumu ambapo Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "Jamii ni Chachu ya mabadiliko, tuungane kupunguza maambukizi, mapya ya VVU"

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.