ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, November 20, 2019

MAHOJIANO YA KWANZA YA JOSE MOURINHO BAADA YA KUJIUNGA TOTTENHAM


Mapema leo klabu ya Soka ya Tottenham imemtangaza Kocha raia wa Ureno, Jose Mourinho kuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo baada yakumtimua aliyekuwa Kocha wake, raia wa Argentina Mauricio Pochettino.

Mara baada ya kukabidhiwa jukumu la kukinoa kikosi cha  Tottenham inayoshiriki Ligi kuu ya Soka ya Uingereza (EPL), kocha Jose Mourinho amefunguka kupitia Sky Sports mtandao wa kijamii wa Twitter na kusema;

“Nina furaha ya kujiunga na club hii yenye historia nzuri na mashabiki wenye moyo na timu yao. Ubora wa kikosi na mfumo wa kukuza vipaji wa club hii unanifurahisha sana. Kwenda kufanya kazi na wachezaji ambao wananivutia inapa hamasa zaidi” amesema.


Tottenham inakuwa timu ya tatu ya Uingereza kufundishwa na Kocha Mourinho baada ya awali kuzifundisha Manchester United na Chelsea.

Mourinho ametajwa kuwa Kocha wa Tottenham akichukua mikoba iliyoachwa na Kocha Mauricio Pochettino kwa kusaini kandarasi hadi mwisho wa msimu wa 2022-23.

Mourinho akiwa Kocha nchini Uingereza alishinda mataji matatu ya Ligi Kuu Soka nchini humo, Kombe la FA mara mbili akiwa na Chelsea, pia alishinda Europa League na Carabao Cup akiwa na Manchester United.



Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.