ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, November 18, 2019

MAREKANI: PELOSI AMTOLEA MWITO TRUM KWENDA KUJIELEZA BUNGENI.

Spika wa baraza la wawakilishi la Marekani Nancy Pelosi, amemtaka rais wa nchi hiyo Donald Trump kuenda katika baraza hilo na kueleza ukweli wake mbele ya kamati inayofanya uchunguzi dhidi ya rais huyo. 
Seneta mwingine Chuck Schumer ambaye kama Pelosi anatoka chama cha Democratic, ameunga mkono wito huo, akisema ikiwa Trump hakubaliani na yanayosemwa katika mchakato wa kumchunguza, badala ya kutuma ujumbe wa twitter anapaswa kujieleza mbele ya kamati ya uchunguzi, tena chini ya kiapo. 
Kupitia mtandao huo huo wa twitter, hivi punde Rais Trump amesema anafikiria kuitikia wito wa Pelosi na kujieleza mbele ya kamati inayomchunguza. 
Haya yanajiri wakati mchakato wa uchunguzi unaoweza kufungua njia ya kumshitaki Rais Trump ukiingia katika wiki ya pili, ukitarajiwa kumkaribisha mtu anayechukuliwa kama shahidi muhimu kuliko wote, ambaye ni balozi wa rais Trump katika Umoja wa Ulaya, Gordon Sondland.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.