ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 1, 2019

WANACHAMA CCM WATISHIA.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya mpanda Abel kimazi ameshindwa kutoa sababu za kutopitishwa jina  la mgombea aliyeshinda kwa madai kuwa  ni siri ya kikao cha chama.

Hata hivyo amedai kuwa chama cha mapinduzi kinafuata katiba kanuni na taratibu katika kufanyia maamuzi hivyo kikao kinauwezo wa kutengua au kumpitisha mgombea aliyechaguliwa na sio kigezo cha kura.

Na Adelina Kapaya, Katavi

Baadhi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Irembo Wilaya ya Mpanda mkoa wa Katavi wametishia kutokushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwa madai ya kupitishwa mgombea wa ngazi ya mwenyekiti wa mtaa  ambaye  hakushinda kwenye kura za maoni .

Paskal kasomo ni mgombea aliyeshinda kwa kura 85 lakini jina  lililopitishwa  ni David sanganzila aliyepata kula 51na kupewa nafasi ya kugombea.

Kwa upande wake paskal kasomo ambaye  alistahili kutetea nafasi hio amesema kuwa hajui sababu zilizofanya jina lake kutopitishwa kwani amefuatilia ngazi ya wilaya na Mkoa lakin hajapewa majibu.

Baadhi ya wakazi wa mtaa huo wamedai kuwa mgombea aliyepitishwa kutetea nafasi hio hana Sifa ndio maana hakushinda kwenye kura za maoni licha ya kupewa nafasi hivyo wameomba kurudishiwa mgombea waliomchagua.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.