ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, September 4, 2019

UJIO WA YANGA KUINUFAISHA MWANZA KIUCHUMI

Mkuu Mkoa Mwanza John Mongela amesema ujio wa timu ya Yanga SC ni fursa ya kibiashara na uchumi kwa mkoa wake.

Mongella ameyanena hayo hii leo (Jumatano ya tarehe 4 September 2019) mapema asubuhi wakati wa kutoa taarifa za ujio wa timu hiyo jijini Mwanza kama sehemu ya maandalizi ya yake kuelekea mchezo wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Zesco ya nchini Zambia.

HALI IMEKUWA VIPI BAADA YA YANGA KUTUA
Baada ya timu ya Yanga Afrika kuwasili leo majira ya saa 9:00 alasiri kwenye Mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza na maeneo ya jirani pilikapilika zilionekana kwa wanachama na mashabiki wa timu hiyo kutumia pikipiki na magari ya kukodi kuongozana kuelekea Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuilaki hali iliyosababisha kufungwa kwa baadhi ya barabara katika Mitaa huku wauzaji wa Jezi za timu hiyo wakitumia fursa hiyo kuuza ili mashabiki hao waweze kusherehesha mapokezi.






Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.