ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 17, 2019

MBWANA SAMATTA AWA MTANZANIA WA KWANZA KUCHEZA UEFA


Leo usiku timu ya Genk anayocheza Mtanzania, Mbwanna Ally Samatta wataanza kucheza mechi ya kwanza kwenye UEFA dhidi ya Salzburg.

Nyota wa Kitanzania na nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta anayekipiga na klabu ya Genk anapata mafanikio makubwa kama Mtanzania kucheza Ligi ya Mabigwa Ulaya.

Samatta akiwa kinara wa mabao msimu uliopita ndani ya Genk aliiwezesha klabu yake kupata nafasi ya kushiriki Uefa Champions League, baada ya Genk kunyanyua kombe la ligi kuu Ubelgiji, hii ni mara ya kwanza Genk kushiriki bila kupitia hatua ya mtoano.

Lakini taarifa mbaya ni kwamba, kunauwezekano wa Samatta kukosa mchezo wa leo dhidi ya Salzburg, kutokana na majeraha ya goti aliyopata kwenye mechi ya Tanzania dhidi ya Burundi kufuzu Kombe La Dunia

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.