ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, September 15, 2019

TAHARUKI: KUNDI LA TEMBO LAVAMIA MAKAO MAKUU YA JIMBO LA WAZIRI MPINA/ WANANCHI WAPAZA SAUTI

KUNDI la Tembo kutoka Pori la Akiba la Maswa (Maswa Game Reserve) lililoko wilayani Meatu mkoani Simiyu limevamia Makao Makuu ya Jimbo la Kisesa mji wa Mwandoya na kuzua taharuki kubwa kwa wananchi wa eneo hilo.

Kundi hilo la Tembo wapatao 34 waliingia katikati ya Kijiji cha Mwandoya ambako shughuli za kiuchumi na kijamii zilisimama kwa muda kufuatia taharuki hiyo huku wananchi wa eneo hilo wakiomba Serikali kuchukua hatua za haraka kuzuia tembo hao wasifike kwenye makazi ya watu kwani ni wanyama wakali wanaweza kuleta madhara makubwa kwa binadamu na uharibifu wa mali.


Pia Wananchi hao wameshukuru Mbunge wa Jimbo hilo, Mheshimiwa Luhaga Mpina kwa hatua aliyochukua ya kuanzisha operesheni ya kuwafukuza tembo hao inayoendeshwa na vijana wa jimbo hilo wakishirikiana na Askari wa Pori la Akiba la Maswa ili kupunguza madhara yatokanayo na wanyama hao

Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Mwandoya Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu, Kibona Jackson Bujoma amesema kundi hilo la tembo lilizua taharuki kubwa na kushukuru kikosi cha doria kilichoundwa Mhe Mpina kuwezesha kuwafukuza tembo hao na kuwarejesha hifadhini bila kuleta madhara kwa wananchi.

Kibona alisema pia tayari Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. Mpina ameshaunda vikundi vya vijana sita kutoka kila kijiji kiichopo kando ya hifadhi hiyo ambapo watakuwa wanashirikiana kufukuza tembo na askari wa Pori la Akiba la Maswa

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.