ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, September 15, 2019

HUYU NDIYE ANSSUMANE FATI - KINDA WA KATALUNYA.

Anssumane Fati ni kijana mdogo mwenye umri wa miaka 16, alizaliwa tarehe 31 October 2002 kule nchini Guinea-Bissau, alijiunga na academy ya Barcelona (La Masia) mwaka 2012.

Mtoto ana balaa kubwa sana huyu ni ingizo moja matata sana ndani ya kikosi cha Barcelona akitokea La Masia.

Jana amepiga goli moja dakika ya pili tu na kutoa pasi kwa Frankie de Jong iliyozaa goli la pili dakika ya saba wakati Barcelona ikiwaangamiza Valencia 5-2 ndani ya Camp Nou.

Ni mtu mwenye kasi, anaweza kumiliki mpira, anapiga mashuti, akiingia kwenye box anakuwa mwiba mkali zaidi. Ni mchezaji wa viwango sana, kama atajitunza na kulinda kipaji na kiwango chake Anssumane Fati anaweza kuja kuwa moja ya wachezaji wakubwa sana ambao majina yao yataimbwa na wazungu muda wote.
Shida sasa wale watu weupe ambao Salamba aliwaomba viatu (utani) tayari wamemshawishi abadilishe uraia wake na muda wowote anaweza kuwa Mhispania. Wakati huo huo wakoloni wa zamani wa Guinea-Bissau Taifa la Ureno nao wameonyesha nia ya kutaka kumshawishi Anssu abadilishe uraia wake na kuchezea timu ya vijana ya nchi hiyo.

Kwa upande wake Anssu yuko tayari kubadilisha uraia na kuwa raia wa Hispania na kama atafanikiwa basi ataanza kukitumikia kikosi cha Hispania katika fainali za Kombe la Dunia kwa vijana chini ya miaka 17 nchini Brazil kuanzia tarehe 26 October mpaka tarehe 17 November 2019.

Anssumane Fati mpaka sasa hajachezea timu ya Taifa lolote hivyo anayo nafasi ya kuchagua ni Taifa gani alitumikie kati ya mataifa matatu ya Guinea Bissau (taifa ambalo amezaliwa), Ureno (taifa lililotawala Guinea Bissau enzi za ukoloni) na Hispania (taifa ambalo ameishi tangu akiwa na miaka 6).

Anssumane Fati anakuwa mchezaji kijana mdogo zaidi wa pili katika historia ya Barcelona kuingia kwenye kikosi cha wababe hao wa Katalunya wa kwanza alikuwa ni Vicenç Martínez mwaka 1941, yeye alianza kuichezea Barcelona mechi ya kwanza akiwa na miaka 16 na siku 280 huku Anssu yeye akiichezea Barcelona mechi ya kwanza ya Laliga akiwa na miaka 16 na siku 298.

Fati ndiye mchezaji kinda zaidi ambaye amecheza mechi katika Ligi Kuu ya Hispania Laliga na kufunga goli la mapema zaidi dakka ya 2 na kutoa pasi ya goli dakka ya 7 katika mechi moja. Amefanya hivyo kwenye mchezo kati ya Barcelona dhidi ya Valencia tarehe 14 September 2019 katika uwanja wa Camp Nou.

Anssumane Fati pia anakuwa mchezaji kinda zaidi wa kwanza mwenye umri wa miaka 16 akitumikia kikosi cha Barcelona (senior team) kufunga goli akiwa na kokisi hicho.

Anssumane Fati alianza maisha yake ya soka pale familia yake ilipohamia nchini Hispania kitongoji cha Herrera katika mji wa Sevilla akiwa na umri wa miaka 6. Wakati kaka yake mkubwa Braima alipojiunga na Sevilla mwaka 2009 yeye Anssumane alikuwa akicheza katika timu za watoto za CDF Herrera mpaka mwaka 2010 alipojiunga na timu za watoto za Sevilla mpaka mwaka 2012. Anssumane Fati alijiunga na academy ya Barcelona La Masia mwaka 2012 na amekuwa akicheza kwenye timu za vijana za Barcelona mpaka tarehe 24 July 2019 aliposaini mkataba wa kuitumikia "Barcelona senior team" mpaka mwaka 2022.

Kijana anajua sana kufunga aisee ndio maana wazungu wameamua kumpa uraia na sasa wanachofanya Barcelona ni kumuanzisha kwenye mechi za La Liga ili aendelee kuwa fiti kabla ya kwenda Brazil kama kila kitu kitakuwa sawa katika dili lake la kuitumikia timu ya Taifa ya vijana ya Hispania.

Anssumane anacheza nafasi ya kiungo wa pembeni namba 11.

Huyo ndio Anssumane Fati chaguo la Ernesto Valverde kinda mwafrika anaepasua vichwa vya wazungu.

Ndimi,
Emmauel M. Makalla.
0716605949

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.