ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 8, 2019

VIDEO:- WAZIRI MKUU AONGOZA UJUMBE WA SERIKALI YA TANZANIA MAZISHI YA MKE WA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI


HATIMAYE Mwili wa Natalia Bahati Kilangi ambaye alikuwa mke wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Professa Adelardus Kilangi umezikwa leo majira ya saa nane mchana nyumbani kwake, Luchelele, wilayani Nyamagama mkoani Mwanza.

 Viongozi mbalimbali wamejitokeza leo Jumatano Agosti 7,2019 katika ibada hiyo inayoongozwa na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Flavian Kasala.

Akiongoza ujumbe wa Serikali Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewasihi viongozi wa dini na wadau mbalimbali kumuombea Professa Kilangi na familia yake kwa kuwa wanapitia katika kipindi hiki kigumu hasa ikizingatiwa kuwa mkewe ndiye aliyekuwa tulizo kwa Profesa Kilangi ambaye amekuwa mshauri mkubwa wa Serikali katika harakati mbalimbali za  Maendeleo. 

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.