ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, August 12, 2019

TANZANIA YATWAA KOMBE LA COSAFA U201 WANAWAKE.


Timu ya taifa ya wanawake chini ya umri wa miaka 20, Tanzanite imefanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Kusini mwa Afrika (COSAFA) baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Zambia leo Uwanja wa Gelvandale mjini Port Elizabeth.

Mabao ya Tanzania inayofundishwa na kocha Bakari Nyundo Shime anayesaidiwa na Edna Lema yamefungwa na Opa Clement dakika ya 24 na Protasia Mbunde dakika ya 87.

Ushindi huo pia ni sawa na kulipa kisasi kwa Tanzanite baada ya kufungwa mabao 2-1 pia na Zambia katika mchezo wa awali, kwenye Kundi B. Ikumbukwe Tanzania iliingia fainali baada ya kuwafunga wenyeji, Afrika Kusini Uwanja wa Uwanja wa Gelvandale mjini Port Elizabeth.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.