ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 30, 2019

Tumia hii tafadhali : MWENYEKITI WA CCMMKOA WA SHINYANGA AZINDUA 'KISHAPU YA KIJANI' AONYA CCM KUWEKA WAGOMBEA WASIOKUBALIKA

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa, amezindua rasmi kampeni ya 'Kishapu ya Kijani', huku akionya viongozi na wanachama wa chama hicho kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ambao utafanyika mwezi Oktoba mwaka huu kutopitisha wagombea wasio na sifa.
Uzinduzi wa kampeni hiyo wilayani Kishapu umefanyika leo Julai 28, 2019  katika kata ya Maganzo kwenye Uwanja wa michezo, na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa CCM, wilaya na mkoa , wanachama, wananchi wakiongozwa na mbunge wa jimbo a Kishapu Suleiman Nchambi.
Mlolwa ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi  amesema lengo la Kampeni ya Kijani ni kuhakikisha kuwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwaka 2020, wagombea wote wa CCM wanashinda kwa kishindo na kutowapatia hata kiti kimoja wapinzani.
Amebainisha kuwa ili adhma hiyo ipate kutimia ni marufuku viongozi wa CCM pamoja na wanachama kupitisha wagombea watakaowania viti vya uongozi kwenye chaguzi hizo, ambao watakuwa hawana sifa na wasiokubalika kwa wananchi, bali wapitishe wagombea wenye vigezo ambao watarahisisha uchaguzi na hatimaye kupita bila ya kupingwa.
“Tunaposema kampeni ya kijani maana yake ni kushinda viti vyote vya ugombea kwenye chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani, na kutowapa nafasi wapinzani sababu CCM ndiyo chama pekee ambacho kinaleta ukombozi kwa wananchi, nadhani mnaona nyie wenyewe mambo anayo yafanya Rais wetu Dkt. John Magufuli,”amesema Mlolwa.
“Hivyo ili tupate kushinda viti vyote vya uongozi ni lazima tupitishe wagombea wote ambao wana sifa na kukubalika kwa wananchi, na siyo kupitisha tu watu ambao hawana vigezo wana maskendo machafu huko kwa wananchi kisa  tu wana pesa, nawasihi msipitishe watu wa namna hiyo watatuangusha,”ameongeza.
Katika hatua nyingine alionya makundi ndani ya chama katika kuelekea kwenye kipindi hiki cha uchaguzi, na kuwataka wawe kitu kimoja katika kuendeleza mapambano ili waweze kupata ushindi wa kishindo, na baada ya hapo, pale penye mapungufu ndipo wakae kuyamaliza na kusameheana.
Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Kishapu Suleimani Nchambi, alimtoa wasiwasi mwenyekiti huyo wa CCM Mkoa wa Shinyanga, kuwa jimbo hilo hakuna mgombea wa upinzani ambaye atashinda kwenye chaguzi zote, kwani wananchi wana imani na CCM kutokana na kuwatekelezea maendeleo yakiwamo maji safi na salama kutoka ziwa Victoria.
Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilayani Kishapu Joseph Kwilasa, amewataka vijana kutotumika kuvuruga amani kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwaka ujao, bali wajiandikishe kwa wingi na kupiga kura kwa kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo ambao wanatoka CCM.
     TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI
Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa akizindua kampeni ya "Kishapu ya Kijani" na kuonya kuweka wagombea wasio na sifa wala kutokubalika kwa wananchi kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM Mkoa wa Shinyanga Barack Shemahonge, akizungumza kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Kishapu ya Kijani.Amewataka vijana kutofanya makosa bali wachague wagombea wote wa CCM, na pia wajiunge kwenye vikundi ili waweze kupata mikopo na kujipatia kipato kuliko kusubili kutumika kwenye uchaguzi na kupewa vitu vidogo.
Mbunge wa jimbo la Kishapu Mhe. Suleiman Nchambi akisalimia wananchi na wanachama wa CCM wilayani humo kabla ya kutoa salamu zake kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Mbunge wa jimbo la Kishapu Mhe. Suleiman Nchambi akizungumza na wananchi wa jimbo hilo kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani, na kuelezea kuwa serikali ya CCM haina mpinzani kwenye chaguzi zote zijazo kwani wametekeleza sehemu kubwa ya ilani ya uchaguzi kwa kutekeleza ahadi zake kwa wananchi ikiwamo kuwaletea maji ya Ziwa Victoria wananchi wa Kishapu.
Diwani wa Kata ya Maganzo wilayani Kishapu Mbalu Kidiga, akizungumza kwa niaba ya madiwani wenzake ambapo amesema kuwa kwenye chaguzi zote zijazo CCM itashinda kwa kishindo na hatimaye kuifanya Kishapu kuwa ya kijani.
Afisa mazingira kutoka mgodi wa Almasi Mwadui Prisca John, akipongeza kampeni ya Kishapu ya Kijani na kuwataka siyo kupata ushindi tu bali hata kijani hiyo waielekeze kwenye kupanda Miti na kuondoa hali ya jangwa wilayani humo. Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM wilayani Kishapu Joseph Kwilasa, akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani.Amewaasa vijana kuacha kutumika kwenye kipindi cha uchaguzi, bali wajiandikishe kwa wingi na kwenda kupigia kura wagombea wa CCM ambao ndiyo watawaletea maendeleo. Awali mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Kishapu Shija Ntelezu akisalimia wananchi na wanachama wa CCM kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Wanachama wa CCM wilayani Kishapu wakiwa kwenye uzinduzi wa  Kishapu ya Kijani na kupewa maagizo ya kupigia kura wagombea wote wa CCM Pamoja na kupitisha wagombea wenye sifa pale watakapokuwa wakipiga kura za maoni. Wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Wanachama wa CCM wilayani Kishapu wakiwa wamebeba mabango kwenye uzinduzi wa Kampeni ya Kishapu ya Kijani, wakitoa ujumbe kwenye Kata ya Mwadui Luhumbo ambayo inatawaliwa na viongozi kutoka  CHADEMA. Wanachama wa CCM wilayani Kishapu wakiwa wamebeba mabango kwenye  uzinduzi wa Kampeni ya Kishapu ya Kijani, wakitoa ujumbe kwenye Kata ya Mwadui Luhumbo ambayo inatawaliwa na viongozi kutoka  CHADEMA. Wanachama wa CCM wilayani Kishapu wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Wanachama wa CCM wilayani Kishapu wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Wanachama wa CCM wilayani Kishapu wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Wanachama wa CCM wilayani Kishapu na baadhi ya wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Wanachama wa CCM wilayani Kishapu wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Burudani za ngoma zikinogesha uzinduzi wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Burudani za ngoma zikiendelea kunogesha uzinduzi huo wa kampeni ya Kishapu ya Kijani. Awali mbunge wa Jimbo la Kishapu Suleiman Nchambi mwenye Shati la njano akicheza ngoma wakati akimsubiri mgeni Rasmi mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa kuja kuzindua kampeni ya Kishapu ya Kijani, na wa kwanza kulia ni Diwani wa Kata ya Maganzo Mbalu Kidigi. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa akifungwa Skafu mara baada ya kuwasili kwenye Kata ya Maganzo wilayani Kishapu tayari kwa kuzindua Kampeni  ya Kishapu ya Kijani. Mbunge wa Jimbo la Kishapu Suleiman Nchambi katikati akiwa na mgeni rasmi mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa wa kwanza kulia wakielekea kwenye tukio la uzinduzi wa Kishapu ya Kijani. Maandamano yakielekea kwenye eneo la uzinduzi wa Kishapu ya Kijani. Mbunge wa Jimbo la Kishapu Suleiman Nchambi (kushoto) akifuatiwa na mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa,Mwenyekiti wa CCM Wilayani Kishapu Shija Ntelezu sambamba na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga Barack Shemahonge, wakisali mara baada ya kuhitimisha uzinduzi wa Kishapu ya Kijani.
Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.