ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, July 22, 2019

RAIS MAGUFULI USO KWA USO NA WAFUGAJI WOTE TANZANIA.

Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa amepanga siku za hivi karibuni kukutana na Wafugaji wote Tanzania kama alivyozungumza na watu wa Madini, wafanyabiashara.

Rais Magufuli amesema hawezi kupotozea changamoto za wafugaji hasa katika kushughulikia maeneo ya kuchungia mifugo yao.

"Nimepanga siku za usoni nitakutana na wafugaji wote wa Tanzania, kama tulivyozungumza na watu wa madini, kama ambavyo tulizungumza na Wafanyabiashara, hatuwezi kuignore changamoto zao hasa katika kushughulikia maeneo ya kuchungia mifugo yao," amesema Rais Magufuli leo Ikulu katika hafla ya kuwaapisha viongozi aliowateuwa hivi karibuni.

"Ng'ombe tunao wengie, mpaka sasa tuna Ng'ombe zaidi ya Million 5.5, nitakaa na wafugaji niwasikilize watoe ushauri wao ili tuweze kuwasaidia wafugaji wa Watanzania ili ufugaji uweze kuleta impact ya uchumi wa nchi yetu."

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.