ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 12, 2019

BARCELONA YALAMBA DUME YAINASA SAINI YA GRIEZMANN.


Klabu ya Barcelona imemsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann baada ya kukubali kulipa ada ya mchezaji huyo 120m euro (£107m).

Griezmann mwenye miaka 28 amesaini mkataba wa miaka mitano amabo unajumuisha kipengele cha 800m euro (£717m) ikiwa ataondoka klabu hiyo.

Griezmann alijiunga Atletico Madrid akitokea from Sociedad mwaka 2014 na kufunga magoli 133 kwenye michezo 256.

Mwaka mmoja uliopita, Juni 2018, alisaini mkataba mpya na Atletico wa miaka mitano, hata hivyo ilipofika mwezi Mei mwaka huu akatangaza kuwa ataihama klabu hiyo katika dirisha la usajili la majira haya ya joto.
Griezmann sasa anakuwa mchezaji wa sita ghali zaidi duniani kusajiliwa nyuma ya Neymar, Kylian Mbappe, Philippe Coutinho, Joao Felix na Ousmane Dembele.
Ameshinda mataji kadhaa na Atletico kama Kombe la Europa, kombe la Super Cup la Uhispania, pamoja na Uefa Super Cup.
Pia amekuwa kinara wa magoli wa klabu hiyo katika misimu mitano iliyopita klabuni hapo.
Griezmann anakuwa mchezaji wa nne mkubwa kusajiliwa na Barcelona katika dirisha hili la usajili baada ya kiungo Frenkie de Jong kutoka Ajax, golikipa Neto kutoka Valencia na beki Emerson kutoka klabu ya Atletico-MG ya Brazil.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.