ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, June 7, 2019

THAILAND: WAZIRI MKUU AHUKUMIWA MIAKA MIWILI JELA.

Waziri Mkuu wa zamani wa Thailand, Thaksin Shinawatra amelihukumiwa  kifungo cha miaka miwili gerezani, adhamu hiyo ilitolewa siku ya jana na Mahakama kuu nchini humo.

Bwana Thaksin Shinawatra  ametiwa hatiana kwa kosa la kuzindua bahati nasibu haramu ya serikali zaidi ya miaka kumi iliyopita na kuisababishia serikali hasara.

Majaji wa mahakama kuu ambao ni wasimamizi wa kesi za kisheria dhidi ya makosa ya jinai ya wanasiasa walimhukumu waziri mkuu wa zamani kwa kumpata na hatia ya kuhusika katika uzinduzi wa bahati nasibu haramu ya serikali ambayo inadaiwa ilisababisha hasara ya dola za Marekani milioni 53.8 kati ya mwaka wa 2003 na 2006.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.