ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 6, 2019

MWENGE WA UHURU KUANZA KUIMULIKA MWANZA MEI 14/2019



KWA mara ya kwanza Mwenge wa Uhuru uliwashwa Tanganyika Desemba 9 mwaka 1961. Alexander Nyirenda ndiye aliyepandisha Mwenge juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro kama ishara ya Uhuru na Mwanga.

Mwenge uliwashwa kama ishara ya kuangaza ndani na nje ya nchi kuleta matumaini pale yalipopotea, kuleta upendo kwenye uadui na kuleta heshima kwenye chuki.

Tangu kuasisiwa kwa Mwenge wa Uhuru umekuwa ni utamaduni wa kukimbiza mwenge kila mwaka katika mikoa na wilaya mbalimbali za Tanzania.


Safari hii mbio za mwenge kwa mkoa wa Mwanza zitaanza tarehe 14 Mei 2019 ambapo Misungwi ndiyo wametunukiwa hadhi ya kuulaki.

Swali linabaki pale tulipoishia....Jeh safari hii ukimulika, atapona mtu?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.