ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 6, 2019

LIPULI YAILIPUA YANGA


Kocha Mkuu wa Yanga SC,  Mwinyi Zahera amesema kuwa malengo ya kuchukua ubingwa wa FA yalikuja katikati ya msimu, kutokana na hali ya timu yao walikuwa wakipambana wasimalize chini ya nafasi ya 10 katika ligi kuu.

Ametoa kauli hiyo mara baada ya kikosi chake kufungwa goli 2-0 na Lipuli FC na kutolewa kwenye michuano ya kombe la Shirikisho la Azam Sports Federation Cup (ASFC).

"Tulipaswa kumaliza Ligi nafasi ya sita au ya saba kutokana na hali ya timu, tukasema tufanye nguvu tusimalize chini ya 10 na hdi leo tunaongoza Ligi" amesema.

Ameendelea kwa kusema, "FA ilikuja katikati ya Ligi, ndio tukasema sio mbaya tunaweza kubeba kikombe cha FA tukaaza kutia nguvu".

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.