ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, May 6, 2019

HII HAPA BEI MPYA YA PAMBA.

Msimu mpya wa ununuzi wa Pamba umezinduliwa rasmi, huku Serikali ikitangaza bei mpya ya shilingi 1200 kwa kilo moja ya zao hilo ikiwa ni ongezeko la shilingi 100 kwa kilo ikilinganishwa na bei ya shililingi 1100 msimu uliopita.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi bwana Amosi Makala, amesema Serikali imekusudia kuongeza bajeti ya sekta ya kilimo ili kuwahakikishia wakulima kunakuwa na upatikanaji mzuri wa pembejeo na huduma ya ugani kwa lengo la kuongeza tija na mapato.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba(TCB), Marko Mtunga amesema bodi hiyo inatekeleza mikakati ya kuongeza tija kutoka kuzalisha kilo 300 kwa hekari hadi kfikia kilo zaidi ya 1,000.

Amesema licha ya changamoto kadhaa za uzalishaji wa pamba nchini, msimu huu unatarajiwa kuongeza hadi zaidi ya tani 400,000 kutoka zaidi ya tani 200,000 za msimu uliopita.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.