ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, May 24, 2019

AIRPORT SIO UCHOCHORO WA KUPITISHA MAGENDO - IGP Sirro



Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP,  Simon Sirro amesema kuwa, maeneo ya viwanja vya ndege hususani kiwanja cha ndege Dar es salaam kamwe hakitakuwa uchochoro wa kupitisha na kusafirisha magendo, biashara ya binadamu, nyara za serikali pamoja na dawa za kulevya.

IGP Sirro ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) Terminal III kwa lengo la kujionea maendeleo ya ujenzi wa kiwanja hicho ambacho hadi sasa ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 99.

Aidha, IGP Sirro, amesema kuwa, Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha hali ya usalama inakuwepo kiwanjani hapo na kwamba hakuna mtu atakaye jaribu kuutumia uwanja mpya wa ndege terminal III kwa vitendo vya kuhujumu uchumi wa taifa letu.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.