ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 12, 2019

KATIBU WA IPC:WAANDISHI WA HABARI ACHENI KUWA MAAFISA HABARI

Katibu wa Iringa Press Club (IPC),Tukuswiga Mwaisumbe akiongea na mwandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani yatakayofanyika siku ya tarehe 03 / 05 / 2019


NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

WAANDISHI wa habari mkoani Iringa wametakiwa kuacha kuandika habari kama maafisa habari wakati kunachangamoto nyingi ambazo zinawakabili wananchi ambazo zinahitaji kutafutiwa ufumbuzi wa kina.

Akizungumza na blog hii Katibu wa Iringa Press Club (IPC),Tukuswiga Mwaisumbe alisema kuwa waandishi wengi waandika habari za mialiko kuliko kuandika habari za kichunguzi ambazo zinatija kwa taifa kwa maendeleo ya nchi.

“Kwetu waandishi wa habari tumekuwa tukisubilia kupewa habari na viongozi mbalimbali na ndio maana tumekuwa tunaandika wanachotaka wao lakini sio waandishi hapo zamani tulikuwa tunauwezo wa kuhoji kutokana na changamoto za wananchi” alisema Mwaisumbe

Mwaisumbe alisema kuwa jukumu kubwa la waandishi wa habari ni kukusanya na kuzichakata na kuzichapisha habari na kumekuwa na changamoto kubwa ni kukusanya habari kutokana sheria mbalimbali ambazo zimetolewa hivi karibuni.

Kuna sheria kandamizi kwa waandishi wa habari ambazo zinasababisha waandishi wa habari kuwa maafisa habari kutokana na sheria zifuatazo,Sheria ya mitandao ya kijamii,sheria ya takwimu,sheria ya upatinaji wa habari na sheria ya huduma kwa vyombo vya habari 

“Sheria hizi zimekuwa kikwazo kwa waandishi wa habari kutokana na kanuni zake jinsi zilivyo na zinavyofanya kazi mfano sheria ya huduma kwa vyombo vya habari inamruhusu kama wa polisi kuchukua vifaa vya habari na kukaanavyo hadi atakapo maliza uchuguzi wake hizo ndio changamoto zilizopo” alisema Mwaisumbe

Mwaisumbe alisema kuwa mwandishi wa habari ni kiungo muhimu katika ya wananchi na viongozi mbalimbali kwa kuwa anachujukumu na kufichua changamoto za wananchi na kuzifikisha kwa viongozi kwa lengo la kutatua changamoto hizo.

Mwandishi anajukumu la kutafuta changamoto za wanachi na kuzifikisha kwa viongozi kwa namna ambavyo anafanya kazi kwa lengo la kusaidia kutatua changamoto hiyo,na ndio maana ya mwandishi kuwa daraja kati ya wananchi na serikali.

Mwaisumbe alisema kuwa kwa mfumo uliopo hivi sasa imekuwa vigumu mno kumpata kiongozi hasa viongozi wa kiserikali kujibia zile kero ambazo umezifumbua kwa wananchi kwa hiyo ni changamoto kubwa kwa waandishi katika kipindi hiki.

“Unaweza ukamtafuta kiongozi furani kujibia kero za wananchi huwezi kupata huo muda labda ajisikie yeye lakini kiongozi huyo akiwa na shida na vyombo vya habari atawaita kwa muda wake tena kwa kujisia yeye mwenyewe huu ndio mfumo ambao tunao hivi sasa” alisema Mwaisumbe

Mwaisumbe alimalizia kwa kuwasema kuwa kwa sasa habari za radio,televiseni na magazeti kwa sasa habari zote zinahabari zote zinazofanana kutokana na sheria zilizopo ambazo zinamfunga mwandishi kutanua wigo wake wa uandishi

“Kama nilivyosema hapo awali kuwa habari nyingi hivi sasa hazina radha ile inayotakiwa kwa walaji wa habari hivyo ipo siku taaluma hii itakufa kwa kuwa wanaofanya habari za kichunguzi hazipo tena” alisema Mwaisumbe

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.