ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, April 18, 2019

BODABODA 8 WASHIKILIWA POLISI KWA TUHUMA ZA MAUAJI YA ASKARI.


Na, Clavery Christian Bukoba.

Jeshi la Polisi mkoani Kagera linawashikilia waendesha pikipiki 8 maarufu bodaboda kwa kumshambulia kwa kipigo kikali MG.433651 Steven Sospeter kilichopelekea kupoteza maisha.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera amesema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake ambapo amesema kuwa MG Steven Sospeter mhaya, miaka 37 ambaye alikuwa askali mgambo na mkaazi wa Gera alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa kupigwa na fimbo, mawe, ngumi na mateke sehemu mbalimbali za mwili wake na kundi la bodaboda baada ya marehemu kutuhumiwa kuiba pikipiki MC.799 BZY aina yaBajaji Boxer rangi nyekundu mnamo tarehe 15/04/2019 majira ya saa 21:00 usiku.

Malimi amesema kuwa Steven na wenza ke wawili wakiwa kazini eneo la kizuizi barabarani iliyopo kijiji cha Gera walimkamata Justine Jackson mhaya miaka 20 ambaye ni bodaboda na mkazi wa kyakakombo akiwa na pikipiki hiyo MC 799 BZY akiwa anasafirisha mkaa gunia mbili kwenda bukoba mjini bila kibali ambapo walimkamata na kumpa maelekezo ya kulipia faini ambapo kijana huyo alikosa pesa ya kulipia faini na kuamua kukaa na pikipiki hiyo mpaka asubuhi na ilipofika asubuhi ya tarehe 16/04/2019 ambapo marehemu alichukua pikipiki hiyo na kuonda nayo kwa ajiri ya kwenda kuikabidhi bunazi kwenye ofisi ya wakala wa mistu na ndipo alipovamiwa na bodaboda hao akiwa amefika eneo la kajunguti na kumrudisha hadi eneo la mto nkenge na kuanza kumpga hadi kupoteza fahamu ambapo polisi walikuja kumuokoa.

Kamanda Malimi amesema kuwa Polisi walimpeleka kituo cha polisi kyaka na kufungua kesi ya kujeruhi kisha kumpeleka katika kituo cha afya BUNAZI na kulazwa lakini hali yake ilizidi kuwa mbaya na hatimaye Aprili 17 mwaka huu alifariki dunia ambapo amesema kuwa chanzo cha tukio hilo ni bodaboda kujichukulia sheria mkononi.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.