ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, April 21, 2019

KISWAHILI SASA CHAPAA - TUMEONGEA NA MTANZANIA ANAYEMLISHA KISHWAHILI



Mtangazaji wa kituo cha radio cha @jembefm kinachomililiwa na Dr Sebastian Ndege @jembenijembe Mr John Jackson jj amekuwa mwalimu mzuri wa lugha ya kiswahili kwa kijana mdogo na  mchambuzi wa soka la kimataifa anayeendelea kujizolea umaarufu nje na ndani ya Afrika Mashariki  

Kwa kuongea kiswahili hasa anapofanya uchambuzi wake wa soka @braydonbentpage amejizolea umaarufu baada ya vipande vyake vya video za uchambuzi wa soka  vikitumia baadhi ya maneno ya kiswahili.

Pamoja na kufanya uchambuzi wa soka amewashangaza wana Afrika Mashariki pale  kijana huyo aliposikika  akivitaja vivutio vya utalii vya nchini Tanzania kama Serengeti, Kilimanjaro na Ngorongoro, Kutoka kwenye ukurasa wa Instagram wa Waziri wa maliasili na Utalii Wazuri Dr Hamis Kingwangalla, amemuomba mchambuzi huyo wa soka wakimataifa awe balozi wa masuala ya Utalii na  kumpa ofa kijana huyo kuja kutembelea mbuga zetu za wanyama nchini Tanzania, Pongezi Kubwa kwa wizara maliasili na Utalii kwa kuliona hili na kulibeba.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.