ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 24, 2018

WANANCHI NA WADAU WA MAENDELEO WAHAMASISHA KUCHANGIA MFUKO WA UDHAMINI WA UKIMWI.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mkoani  Dodoma  Bw. Jabir  Shekimweri akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge wakati wa hafla ya kuhamasisha na kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF), hafla hiyo imetanguliwa na matembezi ya hisani yaliyofanyika Jijini Dodoma leo yakishirikisha  wananchi,  wanafunzi  na wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI.
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI  (TACAIDS) Dkt. Leonard Maboko akizungumzia mambo yatakayofanyika kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani ikiwemo wiki ya maonesho itakayoenda sambamba na kuanzishwa kwa jiji cha vijana ndani ya uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma ambapo vijana watajifunza masuala mbalimbali ikiwemo Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Upimaji wa Virusi vya UKIMWI, Ushauri nasaha, upimaji wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama shinikizo la damu na kisukari .
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI  (TACAIDS) Dkt. Leonard Maboko akiteta jambo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI  (UNAIDS) hapa nchini Dkt. Leo Zekeng wakati wa hafla ya kuhamasisha na kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF), hafla hiyo imetanguliwa na matembezi ya hisani yaliyofanyika Jijini Dodoma leo yakishirikisha  wananchi,  wanafunzi  na wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI.
 Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI  (UNAIDS) hapa nchini Dkt. Leo Zekeng  akizungumzia hali ya UKIMWI Duniani ambapo alibainisha kuwa takribani watu milioni 37 wameambukizwa virusi hivyo, hayo yamejiri leo  wakati wa hafla ya kuhamasisha na kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF), hafla hiyo imetanguliwa na matembezi ya hisani yaliyofanyika Jijini Dodoma leo yakishirikisha  wananchi,  wanafunzi  na wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI.
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mkoani  Dodoma  Bw. Jabir  Shekimweri  (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya wananchi walioshiriki katika wa hafla ya kuhamasisha na  kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF), hafla hiyo imetanguliwa na matembezi ya hisani yaliyofanyika Jijini Dodoma leo yakishirikisha  wananchi,  wanafunzi  na wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI.
Kikosi cha Bendi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikiongoza matembezi ya hisani yaliyofanyika Jijini Dodoma leo yakishirikisha  wananchi,  wanafunzi  na wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI kwa lengo la kuhamasisha na kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF).
Sehemu ya washiriki wa  matembezi ya hisani yaliyolenga kuhamasisha uchangiaji wa fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF) , matembezi hayo ya  hisani yamefanyika Jijini Dodoma.
 Mmoja wa wasanii walioshiriki katika hafla ya uchangiaji  fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF) , Bi. Hadhara Charles akionesha umahiri wake katika kumiliki mpira wa miguu wakati wa hafla hiyo iliyotanguliwa na matembezi  ya  hisani yaliyofanyika Jijini Dodoma.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge inayoshughulikia UKIMWI na Madawa ya Kulevya Mhe. Oscar Mukasa  ambaye ni Mbunge wa Biharamulo akizungumzia faida za wananchi na wadau mbalimbali kujitokeza kuchangia mfuko  wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania leo Jiji Dodoma wakati wa hafla ya kuhamasisha na kuchangia mfuko huo, hafla hiyo ilitanguliwa na matembezi  ya  hisani.
Msanii wa Jijini Dodoma Bi. Judith Jenaro akiimba wimbo wa kuhamasisha wananchi kujitokeza kupima virusi vya UKIMWI ili watambue hali zao ili waweze kuchukua  hatua stahiki.
Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa  Mkoani  Dodoma  Bw. Jabir  Shekimweri  (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu wanafunzi walioshiriki katika hafla ya kuhamasisha na kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF), hafla hiyo imetanguliwa na matembezi ya hisani yaliyofanyika Jijini Dodoma leo yakishirikisha  wananchi,  wanafunzi  na wadau mbalimbali wa mapambano dhidi ya UKIMWI.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge inayoshughulikia UKIMWI na Madawa ya Kulevya Mhe. Oscar Mukasa (Kushoto)  ambaye ni Mbunge wa Biharamulo akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia UKIMWI  (UNAIDS) hapa nchini Dkt. Leo Zekeng   mara baada ya hafla ya kuhamasisha na kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa  Udhamini wa UKIMWI  Tanzania (ATF).
(Picha zote na MAELEZO na TACAIDS)

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.