ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, October 4, 2018

RC MAKONDA AKUTANA NA WATENDAJI TPSF, WAWEKA MIKAKATI MADHUBUTI YA KUWASAIDIA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ametembelea ofisi za Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania TPSF na kufanya mazungumzo ya kutafuta namna bora ya kuweka mazingira bora ya kibiashara ilikuondoa kero zinazowakabili wawekezaji na wafanyabiashara jijini humo. 

Miongoni mwa mambo waliyoridhia kushirikiana ni pamoja na utoaji wa elimu ya biashara, usimamizi wa fedha pamoja na namna bora ya kutumia fursa ya 10% za mkopo zinazotolewa na serikali kwaajili ya vijana, Wanawake na walemavu ili fedha hizo ziwe na tija.

Aidha RC Makonda amezungumza ushiriki wa TPSF katika ziara ya Rais Dkt. John Magufuli jijini Dar es salaam ambayo tunaamini itakuwa fursa kubwa kwa sekta zote ikiwemo Biashara, uchumi, afya, elimu, miundombinu na maji ambapo amewahimiza kuitumia vizuri ziara hiyo ili kufikia ndoto ya Dar es salaam kuwa jiji la kibiashara.

Pamoja na hayo RC Makonda ameelezea mpango wa kuweka kitengo cha uwekezaji (one stop center) itakayohusisha watendaji kutoka taasisi za TIC, TRA, TBS, BRELA, Uhamiaji na wadau wote wanaohusika na biashara ilikuondokana na ukiritimba uliokuwa ukipelekea mianya ya rushwa kwa wawekezaji na mwisho wa siku wawekezaji kukata tamaa ya kuwekeza Dar es salaam.

Kwa upande wake mkurugenzi wa taasisi ya sekta binafsi Tanzania TPSF Bwana Godfrey Simbeye amemuahidi ushirikiano wa kutosha kwa RC Makonda katika masuala mbalimbali yanayolenga kuliboresha jiji la Dar es salaam.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.