ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 3, 2018

PANGANI YAANDIKI HISTORIA SIKU YA WAZEE DUNIANI


 NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akila na wazee wilayani Pangani IKIWA ni kilele cha siku ya wazee Duniani ambako kiwilaya yalifanyika kwenye viwanja vya Bomani wilayani humo
 MKUU wa wilaya ya Pangani,Zainabu Abdallah katika akiwa na wakazi wa mji wa Pangani wakati wa maadhimisho hayo
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wazee

Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gipson George akizungumza katika maadhimisho hayo



 Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gipson George kushoto akishirikiana na wananchi wengine kubeba chakula kwa ajili ya kugawa kwa wazee
 Wazee wakipatiwa vipimo
 Wazee wakiwa kwenye maadhimisho hayo

 Sehemu ya wazee wilayani Pangani wakiwa kwenye maadhimisho hayoi
 Sehemu ya vyakula walivyoandaliwa wazee


NA MWANDISHI WETU, PANGANI.

IKIWA ni kilele cha siku ya wazee Duniani kwa wiki nzima iliyopita jana ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Pangani,Mbunge wa Jimbo hilo na Halmashauri imefanya kampeni ya “Nashukuru Mzee” ambayo imeacha alama kubwa na kuandika historia katika wilaya ya Pangani.

Maadhimisho hayo yalifanyika kwenye viwanja vya Bomani Pangani na baadae kujumuika kwa chakula cha pamoja nyumbani kwa Mkuu wa wilaya ya Pangani.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah alisema wanawashukuru wazee hao kwa kazi nzito walioifanya hadi sasa kuijenga wilaya hiyo na Taifa kwa ujumla.

“Kuwapa zawadi ya uhakika ambayo ni sekta ya afya kama jambo muhimu zaidi kwao nyakati hizi ikiwa ni kuhakikisha wazee wote ndani ya siku wanapata vitambulisho vyao vya matibabu bure kama inavyoelekeza sera ya wazee”Alisema.

“Lakini pia matibabu, upasuaji, vipimo na matibabu bure maalumu toka kwa wataalamu ndani na nje ya Pangani kwa wiki hii hadi kilele huku vipimo vya macho na ambao watapatikana na tatizo watapatiwa miwani”Alisema.

Hata hivyo alisema wataendelea kuwajengea uwezo na kuwapa tumaini jipya na mikakati sambamba na kusikiliza changamoto ambazo zinawakabilia

Kwa upande wake,Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso aliitaka jamii kuwaenzi wazee na kuwathamani kutokana na kuwa na mchango mkubwa kwao

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.