ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, October 17, 2018

MBUNGE JIMBO LA NYAMAGANA ATUNUKU VYETI WAHITIMU 66 SHULE YA SEKONDARI NYANZA WADVENTISTA JIMBO LA KUSINI

 Mbunge Jimbo la Nyamagana Mhe. Stanislaus Mabula ametunuku vyeti wahitimu 66 michepuo ya Sayansi, Biashara pamoja na Sanaa mahafari ya tisa shule ya sekondari Nyanza Wadventista Jimbo la Kusini, yenye jumla ya wanafunzi 507 kati yao wasichana 243 na wavulana 264 iliyopo Wilayani Nyamagana.
Akizungumza kwa niaba ya Mbunge Jimbo la Nyamagana Mhe. Stanslaus Mabula, Mwenyekiti wa taasis ya First Community Organizations Ndg. Ahmed Misanga ametoa salamu za Mbunge ambaye yupo safarini nchini Ujerumani Kikazi, amewapongeza wahitimu kwa kuhitimu kidato cha nne. 

Na kuwaasa kutumia elimu hiyo kuisadia jamii na kujiendeleza kimasomo hadi kufikia daraja la stashahada, shada, shahada ya Uzamili hadi shahada ya Uvamivu. Mhe. Mabula amenituma niwaambie anawatakia maandalizi mema ya mitihani kufuzu kidato cha nne wanafunzi wote wa wilaya yetu ya Nyamagana pamoja na Tanzania nzima mnamo tarehe 5 Ndg Misanga amesema.

Wahitimu wakisoma Risala kwa mgeni rasmi mbali kwa kuainisha mafanikio waliyoyapata ikiwa ni pamoja na maadili mema, stadi za kazi na elimu ya darasani kwa uwiano wa Mwalimu 1 wanafunzi 20 kadharika wamewasilisha ombi la kusaidia kutatuliwa changamoto ya ukosefu wa Bwaro la Chakula pamoja na jengo la Makitaba.

Mahafari haya ya tisa yalipambwa na maonesho maalum ya kazi za wanafunzi, upandaji wa miti. Yalihudhuliwa na Katibu wa Mbunge Jimbo la Nyamagana, mkuu wa shule Sosthenes Malegesi Mgunda, Mkurugenzi wa shule Isaacs Manyonyi, pamoja na wageni mbali mbali waalikwa Mwalimu chuo kikuu cha Arusha Paul Semba, Afisa elimu wilaya na kata, Mtendaji kata pamoja na Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Mahina kati.


 








Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.