ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 19, 2018

MASAUNI AZISHUKIA SHULE ZENYE MAGARI MABOVU ZANZIBAR

 Naibu   Waziri   wa   Mambo   ya   Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti waBaraza la Taifa la Usalama  Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati   ya   Uzinduzi     wa   Kampeni   Maalumu    ya   Usalama   Barabarani  na Udhibiti     wa     Ajali     katika     Uwanja     wa   Skuli   ya   Jang’ombe,   leo   VisiwaniZanzibar. Picha na  Wizara  ya Mambo ya Ndani  ya Nchi.

 Mwanafunzi   wa   Shule   ya   Msingi   Jang’ombe, Aisha Abdallah Haji, akiulizaswali  linalohusiana  na  uvukaji  wa  barabara kwa watu wenye ulemavu wakatiwa   Uzinduzi   wa    Kampeni   Maalumu   ya Usalama Barabarani na Udhibiti waAjali katika  Uwanja  wa  Skuli  ya  Jang’ombe, iliyozinduliwa  leo Naibu Waziriwa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae  pia  ni  Mwenyekiti  wa  Baraza la Taifa laUsalama   Barabarani,   Mhandisi   Hamad   Masauni   (hayupo   pichani),   VisiwaniZanzibar. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Wanafunzi  wakifurahia  jambo wakati  Naibu  Waziri  wa  Mambo  ya  Ndaniya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani,Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani), akizungumza   baada   ya   kuzinduaKampeni   Maalumu   ya   Usalama    Barabarani   na     Udhibiti wa  Ajali   katikaUwanja wa Skuli ya Jang’ombe, leo   Visiwani Zanzibar. Picha na Wizara  yaMambo ya Ndani ya Nchi
 Naibu   Waziri   wa   Mambo   ya   Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti waBaraza     la     Taifa     la     Usalama     Barabarani,   Mhandisi     Hamad   Masauni,akimkabidhi   Mwalimu   Mkuu   wa   Shule   ya   Msingi   Jang’ombe,   Tiffy   Mustafa(kushoto),   moja   ya   kikoti   maalumu   watakachokua   wanavaa   wanafunzi watakaoteuliwa     kuwasaidia     wenzao   kuvuka   barabara     baada   ya   kuzinduaKampeni   Maalumu   ya   Usalama   Barabarani   na   Udhibiti   wa   Ajali katika Uwanja   wa   Skuli   ya   Jang’ombe,   leo   Visiwani   Zanzibar.   Picha   na   Wizara yaMambo ya Ndani ya Nchi
Mkurugenzi     wa   Taasisi     inayojishughulisha     na     masuala     ya     usalama barabarani, Pily   Hamisi     Layda   (kushoto)    akimkabidhi    Naibu    Waziri     waMambo    ya   Ndani ya Nchi,  ambae pia  ni  Mwenyekiti wa Baraza  la Taifa laUsalama  Barabarani,  Mhandisi    Hamad     Masauni,   mpango   kazi   wa   KampeniMaalumu   ya Usalama   Barabarani   na   Udhibiti wa Ajali iliyozinduliwa   katikaUwanja wa Skuli ya Jang’ombe, leo   Visiwani Zanzibar. Picha na Wizara yaMambo ya Ndani ya Nchi.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni, amewatadharisha wamiliki wa shule zinazotumia magari mabovu kubebea wanafunzi ikiwa ni kinyume na sheria za usalama barabarani hali ambayo inaweza kupelekea ajali.

Akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Kampeni Maalumu ya Usalama Barabarani na Udhibiti wa Ajali katika Uwanja wa Skuli ya Jang’ombe, Naibu Waziri Masauni aliwataka wamiliki wa shule kuhakikisha wanatumia mabasi imara ili kuepusha ajali na kuwaasa madereva wa magari hayo kufuata sheria za barabarani “Wamiliki wa shule wanatakiwa wafuate sheria kwa kuacha kutumia mabasi mabovu na kujaza wanafunzi kupita kiasi na tutatumia kikosi cha usalama barabarani kuhakikisha wanafunzi wanakua salama muda wote wakiwa wanaenda shule na kurudi nyumbani.

“Nawaagiza askari wa usalama barabarani kusimamia sheria ili wamiliki watakao kiuka sharia hizo waweze kuchukuliwa hatua pamoja na madereva watakaobainika kuendesha magari mabovu ambayo ni hatarishi kwa wanafunzi,” alisema Masauni

Akitoa ripoti ya matukio ya ajali za barabarani Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Shukuru Amir Ally alisema jumla ya ajali 229 zimeripotiwa ndani ya mwaka huu tofauti na mwaka 2017 ambapo jumla ya ajali 391 zikiripotiwa huku akitoa siri ya kupungua kwa ajali hizo ni ushirikiano wanaoupata kutoka kwa wadau wa usalama barabarani.

Akisoma risala ya uzinduzi huo Mkurugenzi wa Taasisi inayojishughulisha na masuala ya usalama barabarani ya New Vision, Pily Hamis Ladya alisema wamedhamiria kufikia mikoa yote ya Zanzibar na katika awamu hii ya kwanza wanaanza na shule kumi huku akiahidi kuzifikia shule zote katika kutoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi.

“Tunategemea kutoa elimu hii ya usalama barabarani ili kuweza kuwaepusha na kuwalinda wanafunzi wetu na majanga ya barabarani ili waweze kwenda shule na kurudi nyumbani salama,”  alisema

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.