ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, October 4, 2018

SUMATRA YAFUNGUKA KUHUSU VISHOKA, WAMILIKI WA KAMPUNI WAPEWA NENO.





Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa majini na nchi kavu SUMATRA jijini Mwanza umefunguka sababu za kusimamisha ruti kwa baadhi ya barabara huku wakikatiza ruti ndefu kwa gari ambazo hazina uwezo wa kubeba abiri 25.

Akizungumza na wandishi wa habari leo, Meneja wa Sumatra jijini humo, Gabriel Anthony amesema wao kama wenye mamlaka ya udhibiti wa usafiri wanayo mamlaka ya kulinda maslahi ya watoaji huduma wenye ufanisi pamoja na maslahi ya watumiaji huduma huku akisema wanayo jukumu la kutoa na kufuta leseni za usafirishaji.

 Anthony amesema Sumatra imepambana kuhakikisha inamaliza tatizo la vishoka ambao wamekuwa wakichukua leseni jambo ambalo lilikuwa linasababisha utapeli kwa wananchi huku akisema kwa sasa mmiliki au mfanyakazi mwenye kitambulisho cha kampuni ndio watapatiwa leseni za usafirishaji pekee.

" Siku hizi lile suala la mtu mmoja anakuja kuchukua leseni 50 au 100 halipo tena, na nitoe rai kwa wamiliki wa kampuni za usafirishaji kutokubali kuchukuliwa na vishoka na badala yake wafike wenyewe Sumatra na watahudumiwa kwa bei za kawaida kulinganisha na zile wanazotoa kwa vishoka," amesema Meneja huyo wa Sumatra.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.