ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 22, 2018

IDADI YAONGEZEKA AJALI KIVUKO CHA MV NYERERE



GSENGOtV
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Issack Kamwelwe amesema uokoaji wa miili ya waliofariki dunia baada ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere utakamilika leo Septemba 21, 2018 kabla ya saa 12 jioni. 

Kamwelwe ametoa kauli hiyo leo mchana wakati akiwa eneo la tukio Kisiwa cha Ukara wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza. 

Mpaka sasa miili zaidi ya 131, imepatikana huku waliookolewa wakiwa hai 38 ambao wamekimbizwa kituo cha afya Bwisya.


Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella yuko wilayani hapa kuratibu zoezi zima.

Simanzi na huzuni ndizo zilizotawala  katika kisiwa cha Ukara  Wilayani Ukerewe Mkoani Mwanza kufuatia ajali mbaya ya kivuko cha Mv Nyerere kilichokuwa kinafanya safari zake kutoka Bugorora kwenda Kisiwa cha Ukara  kupinduka na kuzama ndani ya Ziwa Victoria mita 100 kabla ya kufika kisiwani hapo.
Siku ya pili sasa Zoezi la uokoaji wa miili ya marehemu linaendelea ambapo hadi sasa zaidi ya miili 100 imeokolewa huku juhudi za utambuzi wa miili hiyo nazo zikiendelea.
Mkuu wa jeshi la Polisi nchini Saimoni Sirro anaeleza juhudi za uokoaji zinazoendelea na kuwatoa hofu wananchi kuhusu miili iliyosalia.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.