ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 22, 2018

INASIKITISHA - KINACHOENDELEA SHUGHULI ZA UOKOAJI AJALI MBAYA YA MV NYERERE KATIKA PICHA

GSENGOtV

Idadi ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere kilichozama juzi mchana Septemba 20, 2018 imefikia 209

Hayo yamebainisha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe  leo jioni Jumamosi Septemba 22, 2018, alipozungumza na waandishi wa habari katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe, Kamwelwe amesema watu waliopatikana wakiwa hai ni 41, baada ya mmoja kuongezeka leo ambaye ni mhandisi wa kivuko hicho, Alphonce Charahani.

Waziri Isack Kamwelwe amesema miili iliyotambuliwa ni 172, kati ya hiyo 112  tayari imeshachukuliwa na ndugu kwa ajili ya maziko.

“Miili 37 bado haijatambuliwa, nieleze tu kuwa ndugu wanaochukua miili kwa ajili ya maziko wanapatiwa ubani wa Sh500,000 kama ambavyo Serikali imeahidi,” amesema Kamwelwe.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Mwanza  John Mongella amesema meli ya MV Nyehunge kutoka Mwanza inaelekea kisiwa cha Ukara ikiwa na vifaa maalum vitakavyotumika kukinyanyua kivuko hicho ili kurahisisha uokoaji na taratibu nyingine.

Kazi ya uokoaji ililejea tena mapema leo asubuhi majira ya saa 12:30
Maskauti pamoja na vijana toka JKT wamefanya kazi ya kipekee hapa Ukara.
Kikosi cha wazamiaji toka shule ya uokoaji Mwanza nacho kiko eneo la tukio.
Mazingitra na jiografia ya eneo la ajali.
Kutoka njia kuu ya kuingia ufukwe wa Bwisya hapa Ukara hii ndiyo jiografia.
Tayari miili kwa ndugu jamaa na marafiki wa marehemu waliowatambua imekwishaanza kuchukuliwa baada ya utambuzi kufanyika.
Uokoaji unaendelea kufanyika...ingawa ni zoezi gumu.
Kwa karibu zaidi....
Pilika pilika eneo la ajali.
Toka hospoitali ya Bwisya hapa Ukara hali halisi na mazingira, hakuna jinsi.
Vikosi kazi.

Mazingira barabara kuelekea Kituo cha afya Bwisya hapa Ukara.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.